CHONGOLO: TANZANIA INAKOPA KWA AJILI YA MAENDELEO, TUSIPOTOSHWE

Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Ndg. Daniel Chongolo amesema Tanzania haina mzigo wa Madeni kama ilivyo kwa mataifa mengine ya Afrika Mashariki, tuwapuuze watu wanaobeza mpango wa Serikali kukopa Fedha Nje ya Nchi, kwani hatua ya Serikali kukopa ni kuendelea Kuijenga Tanzania ili iwe imara Kiuchumi kama ilivyo kwa mataifa yaliyopiga hatua Kimaendeleo.